Dira na Dhamira

SISI NI AKINA NANI?
Sisi ni Chama cha Walipakodi Tanzania (TATA), ni asasi huru isiyo ya kibiashara, isiyoegemea upande wowote, inayojitolea kulinda haki za walipakodi na kuonesha umuhimu wa mchango wao kiuchumi na kijamii katika ujenzi wa Tanzania yenye ushindani .

MAJUKUMU YETU
Kazi ya Chama cha Walipakodi Tanzania (TATA) zinaongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1997, inayoweka umuhimu mkubwa katika ushirikishwaji wa vikundi vya kijamii katika maendeleo ya nchi.
Asasi hii imeanzishwa kwa madhumuni ya kuwaleta pamoja walipakodi wa Tanzania Bara, kulinda na kutetea maslahi yao, kuwashauri na kuwafundisha kuhusu masuala ya kodi. kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari. Tunatetea kuhakikisha, kuwa walipakodi wanakuwa na uelewa mpana wa masuala ya kodi,vilevile kuhaikikisha sheria na sera za kodi, ni za haki na zinaeleweka kiasi ili kuwa na usawa na unafuu wa ulipaji kodi, ukusanyaji kodi wa kiungwana, kujenga mazingira ya maridhiano baina ya walipakodi na Mamlaka za mapato pamoja na kuhamasisha uwajibikaji wa serikali katika matumizi stahiki ya fedha zitokanazo na kodi zinazolipwa na wananchi.

Dira

We envion a fair and transparent tax system in which taxpayers’ rights are protected, driving accountability and good governance.

Dhamira

To champion the advocacy and protection of taxpayers’ rights by enhancing tax compliance, influencing policy, resolving disputes, and advancing government accountability through engagement, advocacy, research, and public education.