Haki za mlipa kodi

Haki za Walipakodi

Haki za mlipakodi huweka pamoja haki zilizopo katika msimbo wa kodi katika haki fulani za kimsingi (Kiungo cha kifungu kifuatacho cha sheria za kodi Tanzania). certain fundamental rights and makes them clear, understandable, and accessible.

Kanuni

This part consist of regulations made by the Minister for matters authorized to be made or prescribed and for better carrying into effect of the principles, purposes and provisions of the respective Acts.

Haki za Walipakodi

  • Haki ya kupata taarifa
    Walipakodi wanayo haki ya kupata taarifa, kujua wanatakiwa kufanya nini ili kufuata sheria, wanatakiwa kupata ufafanuzi unaoeleweka wa sheria na taratibu za TRA hususan za kodi zote pamoja na taratibu za uwasilishaji wa ritani za kodi , ili waweze kulipa kodi kwa kiwango kinachotakiwa. Wana haki ya faragha na usiri kwa shughuli za kibinafsi na za Biashara.
  • Haki ya kupata huduma bora
    Walipakodi wanayo haki ya kupata usaidizi wa huduma bora wa haraka na wa kitaalam toka TRA , kwa kuzingatia taratibu na kanuni za Usimamizi wa kodi ambao unaruhusu mahusiano yanayoeleweka kwa urahisi, na kuwasilisha malalamiko kupitia Tovuti ya TRA juu ya kutoridhishwa na huduma inayotolewa kwao na watendaji wa TRA ili kuimarisha Usimamizi wa kodi.
  • Haki ya kulipa kodi stahiki isio na upendeleo
    Walipakodi wanayo haki ya kudhaniwa kuwa ni waaminifu na kulipa kiasi kile tu cha kodi wanachostahili kulipa kisheria.
  • Haki ya pingamizi dhidi makadirio ya kodi yanayotolewa na TRA .
    Walipakodi wanayo haki ya kuthaminiwa na kusikilizwa wanapotoa pingamizi dhidi ya makadirio ya kodi au uamuzi wowote uliofanywa na mamlaka ya Mapato Tanzania kwa mujibu wa sheria. Lazima kuwasilisha taarifa ya pingamizi kwa maandishi kwa Kamishna ndani ya siku 30, tangu tarehe ya kupata notisi ya makadirio, aeleze kwa usahihi sababu za pingamizi kwa kutoa nyaraka za ushahidi juu ya hoja yake. Na kupokea majibu iwapo TRA haikubaliani na msimamo wao. Hata hivyo pingamizi litakubaliwa pale ambapo mlipakodi amelipa kiasi chote cha kodi kisicho na mzozo au theluthi ya kodi aliyokadiriwa kiasi chochote kikubwa, ndani ya siku thelathini kutoka siku ya notisi ya makadirio. Endapo mlipakodi hataridhika anaweza kupeleka pingamizi kwenye Bodi ya Rufaa ya Kodi kwa uamuzi. Mlipakodi ana haki ya kupata haki mpaka atakapothibitishwa ana hatia.
  • Haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa TRA kwenye Bodi huru.
    Mlipakodi ambaye hajaridhishwa na uamuzi wa pingamizi la Kamishna Mkuu anaweza kukata rufaa kwa Bodi kwa mujibu wa Sheria ya Rufaa ya Mapato ya Kodi. Walipakodi wana haki ya kukata rufaa ya Usimamizi wa haki bila upendeleo katika maamuzi mengi ya TRA ikiwa ni pamoja na adhabu nyingi, na wana haki ya kupokea kwa maandishi jibu kuhusu uamuzi wa Ofisi ya Rufaa. Kwa ujumla wana haki ya kupeleka kesi zao mahakamani
  • Haki ya mwisho wa ripoti ya ukaguzi
    Walipakodi wana haki ya kujua muda wa kawaida, walionao kuhoji msimamo wa TRA pamoja na muda wa juu zaidi ambao TRA inabidi kufanya ukaguzi hesabu za mwaka fulani za kodi. Walipakodi wana haki ya kujua lini TRA inamaliza ukaguzi na kumpatia mlipakodi matokeo ya ukaguzi/mapendekezo baada ya ukaguzi.
  • Haki ya faragha (Privacy)
    Walipa kodi wana haki ya kutarajia kwamba taarifa binafsi au zile za Biashara zitakazotolewa katika ofisi za Mamlaka ya Mapato zitafanyiwa kazi kwa faragha, isipokuwa tu pale sheria itakapoelekeza vinginevyo..
  • Haki ya usiri (Confidentiality)
    Walipa kodi wana haki ya kutarajia kuwa maelezo au taarifa yoyote wanazozitoa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania, (TRA) hazitatolewa nje mpaka pale itakapoidhinishwa kufanya hivyo na mlipakodi mwenyewe au sheria itakapoelekeza kufanya hivyo. Walipa kodi wanahaki ya kutarajia TRA ichunguze na kuchukua hatua stahiki dhidi ya waajiriwa, watayarishaji wa mahesabu, na wengine ambao wanatumia au kuzitoa taarifa za walipa kodi.
  • Haki ya kuwakilishwa
    Walipa kodi wanayo haki ya kuwa na wawakilishi walioidhinishwa wa chaguo lao kuwawakilisha katika shughuli zao za kikodi na TRA. Wanayo haki ya kuambiwa kwamba iwapo watashindwa kumudu gharama za kuajiri wawakilishi wanaweza kustahili kuomba msaada kutoka Idara ya Huduma ya Msaada wa Kisheria wa TATA
  • Haki ya mfumo wa kodi wenye usawa
    Walipakodi wana haki ya kutarajia mfumo wa kodi kuzingatia ukweli na mazingira ambayo yanaweza kuathiri madeni yao ya msingi, uwezo wa kulipa au uwezo wa kutoa taarifa kwa muda muafaka kuwawezesha kuzingatia.. Walipakodi wana haki ya kupata msaada kutoka TATA Idara ya Utetezi wa Mlipakodi ikiwa wanakumbana na ugumu wa kifedha, Au iwapo TRA hawajamaliza kusuluhisha masuala ya kodi ipasavyo na kwa wakati kupitia njia njia zake za kawaida.
  • Motisha na msamaha chini ya sheria ya kodi
    Mlipakodi ana haki ya kupanga masuala yao ya kodi ili kupata motisha na msamaha unaoruhusiwa chini ya sheria za kodi na kutumia fursa za sheria za kodi kwa njia thabiti na ya haki kwa walipakodi wote.

Wasilisha mapendekezo ya mabadiliko ya kodi kwa TATA